13. TAFUTA DAIMA UTAKATIFU
TAFUTA DAIMA UTAKATIFU
1. Tafuta daima utakatifu;
Fanya urafiki na Wakristo tu;
Nena siku zote na Bwana wako,
Baraka uombe kwa kila jambo.
2. Tafuta daima utakatifu;
Uwe peke yako ukimwabudu;
Ukimwangalia mwokozi wako,
Utabadilishwa kama alivyo.
3. Tafuta daima utakatifu;
Kiongozi wako awe Yesu tu;
Katika furaha au huzuni
Dumu kumfuata Yesu Mwokozi.
4. Tafuta daima utakatifu;
Umtawaze Roho moyoni mwako;
Akikuongoza katika haki,
Hufanywa tayari kwa kazi yake.
Comments
Post a Comment