13. TAFUTA DAIMA UTAKATIFU

TAFUTA DAIMA UTAKATIFU

1.  Tafuta daima utakatifu;
Fanya urafiki na Wakristo tu;
Nena siku zote na Bwana wako,
Baraka uombe kwa kila jambo.
 
2.  Tafuta daima utakatifu;
Uwe peke yako ukimwabudu;
Ukimwangalia mwokozi wako,
Utabadilishwa kama alivyo.
 
3.  Tafuta daima utakatifu;
Kiongozi wako awe Yesu tu;
Katika furaha au huzuni
Dumu kumfuata Yesu Mwokozi.
 
4.  Tafuta daima utakatifu;
Umtawaze Roho moyoni mwako;
Akikuongoza katika haki,
Hufanywa tayari kwa kazi yake.

Comments

Popular posts from this blog

18. AKIFA YESU NIKAFA NAYE