Posts

12. EWE ROHO WA MBINGUNI

EWE ROHO WA MBINGUNI 1.    Ewe Roho wa Mbinguni Uje kwetu sasa. Ufanye makazi yako Ndani ya kanisa.   2.    Ndiwe mwanga, umulike Tupate jikana; Mengi kwetu yapunguka, Tujalize, Bwana.   3.    Ndiwe Moto, teketeza Taka zetu zote: Moyo na iwe sadaka Ya Mwokozi, yote.   4.    Ndiwe umande, na kwako Tutaburudika, Nchi kavu itakuwa Ni yenye baraka.   5.    Roho wa Mbinguni uwe Nasi hapa chini, Mwili uufananishe Na Kichwa Mbinguni.

13. TAFUTA DAIMA UTAKATIFU

TAFUTA DAIMA UTAKATIFU 1.    Tafuta daima utakatifu; Fanya urafiki na Wakristo tu; Nena siku zote na Bwana wako, Baraka uombe kwa kila jambo.   2.    Tafuta daima utakatifu; Uwe peke yako ukimwabudu; Ukimwangalia mwokozi wako, Utabadilishwa kama alivyo.   3.    Tafuta daima utakatifu; Kiongozi wako awe Yesu tu; Katika furaha au huzuni Dumu kumfuata Yesu Mwokozi.   4.    Tafuta daima utakatifu; Umtawaze Roho moyoni mwako; Akikuongoza katika haki, Hufanywa tayari kwa kazi yake.

14. YESU KWA IMANI

YESU KWA IMANI 1.    Yesu kwa imani, Nakutumaini, Peke yako; Nisikie sasa, Na kunitakasa, Ni wako kabisa Tangu leo.   2.    Nipe nguvu pia Za kusaidia Moyo wangu; Ulikufa Wewe, Wokovu nipewe Nakupenda Wewe, Bwana wangu.   3.    Hapa nazunguka Katika mashaka, Na matata; Palipo na giza Utaniongoza Hivi nitaweza Kufuata.   4.    Takuwa mzima Nivushe salama Mautini; Sina hofu kamwe Ukiwapo nami Nami nikwandame Siku zote.

15. CHA KUTUMAINI SINA

CHA KUTUMAINI SINA 1.    Cha kutumaini sina Ila damu yake Bwana, Sina wema wa kutosha Dhambi zangu kuziosha.   Chorus: Kwake Yesu nasimma, Ndiye Mwamba: ni salama Ndiye mwamba: ni salama.   2.    Njia yangu iwe ndefu Yeye hunipa wokovu; Mawimbi yakinipiga Nguvu zake ndiyo nanga.   3.    Damu yake na sadaka Nategemea daima, Yote chini yakiisha Mwokozi atanitosha.   4.    Nikiitwa hukumuni, Rohoni nina amani; Nikivikwa haki yake Sina hofu mbele zake.

16. KUMTEGEMEA MWOKOZI

KUMTEGEMEA MWOKOZI 1.     Kumtegemea Mwokozi, Kwangu tamu kabisa; Kukubali neno lake Nina raha moyoni. Chorus: Yesu,Yesu namwamini, Nimemwona thabiti; Yesu,Yesu, yu thamani, Ahadi zake kweli.   2.    Kumtegemea Mwokozi, Kwangu tamu kabisa, Kuamini damu yake Nimeoshwa kamili.   3.    Kumtegemea Mwokozi, Kwangu tamu kabisa, Kwake daima napata Uzima na amani.   4.    Nafurahi kwa sababu Nimekutegemea; Yesu, Mpendwa na Rafiki Uwe nami dawamu.

17. NAMWADAMA BWANA

NAMWADAMA BWANA 1.    Namwadama Bwana kwa alilonena Njia yangu huning’azia; Nikimridhisha atanidumisha Taamini nitii pia.   Chorus: Amini utii, njia pweke ni hii Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii.   2.    Giza sina kwangu wala hata wingu Yeye mara huviondoa Woga, wasiwasi, sononeko, basi; Huamini nitii pia.   3.    Masumbuko yote, sikitiko lote; Kwa mapenzi hunilipia; Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki, Taamini nitii pia.   4.    Mimi sitajua raha sawasawa Ila yote Yesu kumpa; Napata fadhili na radhi kamili, Taamini nitii pia.   5.    Nitamfurahia na kumtumaini, Majumbani na njia-njia; Agizo natenda; nikitumwa hwenda, Huamini nitii pia.

18. AKIFA YESU NIKAFA NAYE

AKIFA YESU NIKAFA NAYE 1.    Akifa Yesu nikafa naye, Uzima upya huishi naye; Humtazama mpaka aje Nyakati zote ni wake Yeye. Chorus: Nyakati zote nimo pendoni, Nyakati zote ni uzimani, Humtazama hata atokee, Nyakati zote mimi ni wake.   2.    Vita sipigi visivyo haki, Na Bwana wangu hapiganiki; Beramu yake haitwaliki, Napo po pote hila sitaki.   3.    Sina mashaka, akawa mbali; Mizigo yote aihimili; Ananituliza Imanweli, Nyakati zote mimi husali.   4.    Sina huzuni na mimi sidhii; Simwagi chozi, wala siguni; Sikuti afa, ila Kitini Daima hunifikiri mimi.   5.    Kila unyonge huusikia; Kila ugonjwa kwake hupoa; Yesu ni mwenye kuniokoa Nyakati zote hunijalia.