19. NDIYO DHAMANA, YESU WANGU

NDIYO DHAMANA, YESU WANGU

1.  Ndiyo dhamana, Yesu wangu;
Hunipa furaha za Mbingu;
Mrithi wa wokovu wake
Nimezawa kwa Roho yake.

Chorus:
Habari njema, raha yangu
Yesu ndiye Mwokozi wangu,
Habari njema, raha yangu
Yesu ndiye Mwokozi wangu.
 
2.  Kumsalimu moyo wangu,
Mara namwona raha yangu;
Aniletea malaika,
Wananilinda, taokoka.
 
3.  Sina kinyume; nashukuru,
Mchana kutwa huja kwangu;
Usiku kucha kuna nuru;
Mwokozi wangu; ndimi huru.
 
4.  Hali na mali anitwaa!
Mara namwona anifaa,
Nami nangoja kwa subira;
Akiniita, nije mara.

Comments

Popular posts from this blog

18. AKIFA YESU NIKAFA NAYE