21. ROHO YANGU HIMA

ROHO YANGU HIMA

1.  Roho yangu hima, na taa yako
Kaiwashe vyema, hapa si pako;
Nguvu zote pia za duniani
Hazitakudhuru ukiamini.

Chorus:
Yesu yuko mbele, Yesu yu nyuma,
Yesu vivyo kando, walindwa vyema.
 
2.  Adui shetani, na nguvu zake,
Bwana ameshinda, kwa kifo chake;
Wewe nguvu huna, huna kabisa,
Ndiwe mpungufu, mnyonge hasa.
 
3.  Toka na mapema, mbele ya wote,
Omba, bisha sana, maisha yote;
Vita vikaliko, macho ukae,
Jivike silaha, nawe sishindwe.
 
4.  Bwana Yesu ndiye kwako Mchunga,
Neno lake Bwana ndilo upanga;
Mbingu zitakwisha, na nchi pia,
Neno lake Bwana laendelea.

Comments

Popular posts from this blog

18. AKIFA YESU NIKAFA NAYE