26. YESU UNIPENDAYE
YESU UNIPENDAYE
1. Yesu unipendaye
Kwako nakimbilia,
Ni Wewe utoshaye
Mwovu akinijia;
Yafiche ubavuni
Mwako maisha yangu;
Nifikishe Mbinguni
Wokoe moyo wangu.
2. Ngome nyingine sina;
Nategemea kwako.
Usinitupe Bwana,
Nipe neema yako,
Ninakuaminia
Mwenye kuniwezesha;
Shari wanikingia,
Vitani wanitosha.
3. Nakutaka Mpaji
Vyote napata kwako;
Niwapo muhitaji,
Utanijazi vyako;
Nao waangukao
Wanyonge wape nguvu
Poza wauguao,
Uongoze vipofu.
4. Bwana umeniosha
Moyo kwa damu yako,
Neema ya kutosha
Yapatikana kwako;
Kwako Bwana naona
Kisima cha uzima,
Mwangu moyoni, Bwana,
Bubujika daima.
Comments
Post a Comment