34. NJONI WENYE DHAMBI

NJONI WENYE DHAMBI

1.  Njoni! njoni! Wenye dhambi,
Njoni, msikawie;
Yesu anawangojea 
Ndiye awapendaye;
Ajuaye awezaye
Kuwaponya ni Yeye.
 
2.  Ewe muhitaji uje;
Anakukaribisha,
Imani, kweli, na toba,
Neema ya kutosha,
Jua sana, kwake Bwana
Bure utayapata.
 
3.  Njoni, mliolemewa
Na dhambi ya Adamu;
Mkingoja kujiponya
Mtapotea mumu;
Si wa haki, ni wakosa
Waoshwao kwa damu.
 
4.  Ikamtokea dhiki,
Mle Gethisemani;
Kisha alipoangikwa
Akalia mtini;
” Imekwisha”, alitosha
Dhabihu ya thamani.
 
5.  Kristo aliye Mbinguni
Hutuombea huko;
Basi mtumai Yeye;
Kamwe mwingine hako
Yesu pweke, Yesu pweke,
Ndiye Mwokozi wako.
 
6.  Wamsifu-sifu sana
Mbinguni malaika,
Wachanganya nyimbo zao
Na waliookoka:
Aleluya wataimba
Waliooshwa taka.

Comments

Popular posts from this blog

18. AKIFA YESU NIKAFA NAYE